Sunday, October 20, 2013

MTANGAZAJI MKONGWE HAPA NCHINI JULIUS NYAISANGA AFARIKI DUNIA LEO 20/10/2013

 Mtangazaji mkongwe hapa nchini Ndg. Julius Nyaisanga a.k.a. Ancle J, ameripotiwa kufariki dunia alfajiri ya  leo 20/10/2013, katika hospitali ya Mazimbu mkoani Morogoro. Akidhibitisha kifo hicho kaimu meneja wa kituo cha Abood Media Ndg. Abeid Dogoli, amesema Julius Nyaisanga ambaye alikuwa mfanyakazi katika kituo hicho kama meneja wa kituo, alipelekwa hospitalini hapo jana mchana akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na presha. Julius Nyaisanga ambaye alishawahi kuwa mtangazaji wa radio tanzania, na radio one, amefariki akiwa na umri wa miaka 53.

MUNGU AILAZE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA NGULI WA UTANGAZAJI UNCLE J. AMEN.

Julius Nyaisanga katikati, akiwa na mtangazaji Liongo wakwanza kushoto, enzi za uhai wake.

No comments:

Post a Comment