Tuesday, October 1, 2013

KAMPUNI YA BANANA YAFANYA MKUTANO NA SHEREHE KABAMBE KWA MAWAKALA WAKE MKOA WA TANGA 2013

 Mkurugenzi mtendaji wa Banana Investments Ndg. Adolf R. Olomi, akitoa semina ya ujasiriamali kwa mawakala wa kampuni mkoa wa Tanga, kwenye sherehe walioandaliwa na kampuni.
 Meneja masoko wa Banana Investments Ndg. David Damian, akitoa somo kwa mawakala mkoa wa Tanga kuhusu utaratibu wa kutoa motisha (Bonus) kwa mawakala wanaofanya vizuri katika mauzo.
 Ngugu Respics Ndukya wakala wa Banana Investments kutoka Korogwe, akiwa ameshikilia Tv bapa yeye na mke wake, ikiwa ni zawadi kwao ya mshindi wa kwanza katika mauzo ya mwaka 2013 kwa mawakala wa mkoa wa Tanga.
 Hapa meneja mauzo wa Banana Investments Ndg. Elisante Makyao, akionyesha baiskeli ambayo ni zawadi ya mshindi wa tatu kwa mawakala mkoa wa Tanga ambaye hakufanikiwa kuhudhuria katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi mtendaji wa Banana Investments, aliyevaa miwani, na meneja mauzo bohari ya Tanga wakimkabidhi Ndg. Materu wa Tanga mjini aliyeshika bahasha zawadi ya TV kichogo, ikiwa ni zawadi ya mshindi wa pili kimauzo kwa mawakala wa mkoa wa Tanga.
 Mmoja wa mawakala mkoa wa Tanga, akipokea zawadi ya saa toka kwa mkurugenzi mtendaji wa Banana Investments, zawadi za saa zilitolewa kwa mshindi wa nne hadi wa kumi na tatu kimauzo.
 Burudani ya muziki pia ilikuwepo, hapa wacheza show wa kundi la promotion la Banana Investments, wakitoa burudani katika sherehe hiyo ya mawakala wa kampuni mkoa wa Tanga.
 Hapa burudani kabambe ikiendelea kutoka kwa mcheza show mahiri Ndg. Tompoo kuwaburudisha wageni.
 Vyakula vya kila aina viliandaliwa, hapa mkurugenzi mtendaji wa Banana Investments akichota chakula kuashiria kuwakaribisha wageni kupata chakula wakati wa sherehe.
 Vinywaji vya kila aina vilikuwepo ndani ya ukumbi, vikiongozwa na vinywaji bora vinavyozalishwa na kampuni ya Banana Investments, ambavyo ni Raha, Raha poa na Fiesta dry gin.

Hapa mawakala wakifurahia jambo wakati wa sherehe yao waliyoandaliwa na kampuni, huku wakifurahia vinywaji bora vinavyozalishwa na kampuni ya Banana Investments.

No comments:

Post a Comment