Yalikuwa ni maandamano makubwa yaliyoandaliwa kupinga uwindaji haramu, na ujangili wa kuua tembo katika nchi ya Tanzania. Maandamano yalianzia kwenye ofisi za Tanapa mjini Arusha na kuhitimishwa kwenye viwanja vya AICC club Kijenge. Waziri wa maliasili na utalii Mh. Hamisi Kagasheki alihutubia wananchi katika viwanja hivyo. Aidha maandamano kama haya yalifanyika katika nchi zingine, ikiwemo China na Marekani kuonyesha kuwa wanapinga ujangili wa tembo duniani. Kampuni ya Banana Investments kwa kutambua umuhimu wa kuhifadhi mali asili za taifa letu, ilishiriki katika maandamano hayo kwa kutuma wawakilishi wake katika maandamano, kama wanavyoonekana kwenye picha hapo chini wakiwa wamevalia t-sheti za kinywa chake cha Fiesta dry gin kinachoongoza katika soko la Tanzania.
No comments:
Post a Comment