Monday, September 30, 2013

Siku wanachama wa Banana Sport Club walipotembelea hifadhi ya Saadani

 Hapa wanachama wa banana sports club wakipata kifungua kinywa katika hotel ya changbay, wakati wa safari yao kuelekea hifadhi ya SAADAN.
 Hapa wakipozi baada ya kifungua kinywa, na kujinunulia mahitaji muhimu njiani wakati wa safari
 Safari ikaanza baada ya kifungua kinywa kuelekea hifadhi ya SAADAN.


 Katika hotel ya Kate iliyoko Korogwe ndipo wanachama wa banana sport club walipopata chakula cha mchana
 Baada ya safari ya kutwa nzima sasa ndani ya saadan, na tayari hapa tent zimeshaandaliwa kwa ajili ya malazi
 Siku iliyofuata safari ya kutembelea vivutio ndani ya hifadhi ilianza. hapa picha ya pamoja kwenye mbuyu uliotumiwa na wajerumani kuwanyongea mababu zetu enzi za ukoloni.
 Hapa baadhi ya wanachama wakijipumzisha baada ya kutoka kutembelea vivutio ndani ya hifadhi
 Baada ya safari kuzunguka hifadhi sasa ni picha ya pozi karibu na bahari ya hindi
 Misosi ilikuwa ya kutosha kabisa, hapa warembo wakijipatia maakuli, ndani ya hifadhi ya saadani
 Mlango huu uliachwa na waarabu waliotumia majengo haya ndani ya hifadhi ya saadani. Mlango huu upo hivihivi tangu mwaka 1700, hadi leo.
 Haya ni mabaki ya stoo iliyotumiwa na waarabu ndani ya hifadhi ya saadani, tangu mwaka 1700.
 Hakika maji ya mto yanatisha. Eneo hili ndipo maji ya mto WAMI yanapokutana na maji ya bahari ya HINDI. wanachama wa banana sport club walitumia boti hii kufika katika eneo hili.
 Ndani ya bahari ya hindi, ilikuwa tukio la kihistoria na la kishujaa kuwa ndani ya maji haya kwa kutumia boti. Hapa boti inapishana na viboko, na mamba.
 Ha.pa nahodha wa boti akiongoza boti, pamoja kutoa maelezo kwa wanachama wa banana sport club
Wengi waliogopa safari hii ndani ya maji, ila walijipa moyo na baada ya kurejea nchi kavu walipongezana kwa kufanikisha tukio hili la kihistoria katika maisha yao.
 Hapa ni kwenye kivuko cha pangani, pia ni eneo maji ya mto pangani yanakutana na maji ya bahari ya hindi.
 Hili ni yai la kasa likiwa limefukiwa kwaajili ya kutotolewa pembeni ya bahari ya hindi ndani ya hifadhi ya saadan. Kasa hutaga mayai nje ya maji na kuyafukia hadi yanapoanguliwa na vitoto hurejea baharini.
 Amini usiamini mnyama Nguruwe huishi katika makazi ya watu ndani ya hifadhi ya saadan, katika kijiji cha saadani.
Katika kivuko cha pangani wakati wakurudi Arusha kutokea hifadhi ya Saadani.


NB: Shukrani ziwaendee waandaaji wa safari hii kwa kuwa na wazo hili na kulifanyia kazi hatimaye kuandaa safari hii. Waliofanikisha safari hii ni MOSES JANUARY na ALBINA ANTHON, hongereni sana. Pia shukrani za pekee ziwaendee viongozi, na wakurugenzi wa Banana investments kwa kuwaruhusu wafanyakazi hao, ambao ni wanachama wa banana sport club, kufanya safari hii. MUNGU AWABARIKI WOTE

Sunday, September 29, 2013

Angalia siku Banana investments waliposhiriki maadhimisho ya Mei mosi 2013 mkoani Arusha

 Hapa bidhaa za Raha, Raha poa, na Fiesta dry gin zinazozalishwa na kampuni bora ya banana investments. Hata afande alivutiwa na bidhaa hizo.
 Wafanyakazi wa kampuni ya banana investments wakati wa maandamano wakiwa wanapendeza na nyuso za furaha.
 Huu ni ujumbe wa mei mosi 2013, ukisisitiza usawa na haki kwa wafanyakazi wa tabaka zote
 Hapa maandamano yakiwa yanaanza, kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa wa Arusha kuelekea uwanja wa Sheihk Amri Abeid, zilikofanyika sherehe.
 Maandamano ya magari, hapa magari ya banana investments yakiwa yanapendeza tayari kwa maandamano
 Burudani ilikuwa ni sehemu ya maadhimisho haya. Hapa wacheza show, pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa banana investments wakiburudisha watazamaji.
                               Magari yakiwa kwenye maandamano
 Kulikuwa pia na maandamano ya pikipiki, hapa wafanyakazi wa banana investments wakiwa na furaha, wakionyesha ujuzi wa kuendesha pikipiki.
 Mmoja wa wafanyakazi wa banana investments akionyesha bidhaa za kampuni, akiwa amependeza kuonyesha furaha ya kushiriki mei mosi.
 Meneja masoko wa banana investments bwana. David Mulokozi, akionyesha ngao ya mshindi wa tatu ambayo kampuni ilishinda kwenye sherehe za mei mosi 2013
 Wafanyakazi wa banana investments wakipata chakula walichoandaliwa na kampuni, kuwapongeza baada ya maadhimisho ya mei mosi 2013
 Hapa wafanyakazi wakicheza muziki wakati wa sherehe kabambe baada ya maadhimisho ya mei mosi 2013. Hapa ni kwenye viwanja wa bustani ya kampuni.
Mkurugenzi wa banana investments akiwahutubia wafanyakazi wakati wa sherehe baada ya maadhimisho ya mei mosi. Aliwashukuru wafanyakazi kwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuiletea kampuni mafanikio.
Unajua kuogelea wewe? Hapa bwana steven mvungi akipiga mbizi ndani ya bahari iliyoko kwenye hifadhi ya SAADAN, wakati wa ziara ya wafanyakazi wa Banana Investments kwenye hifadhi hiyo.
Hiki ni kiwanda cha kutengeneza chumvi kutoka katika maji ya bahari, kinachomilikiwa na wahindi, ndani ya hifadhi ya SAADAN.
Kundi la wafanyakazi wa Banana Investments, wanachama wa Banana sport club, walipotembelea mbuga ya SAADAN. Hapa wakiwa katika picha ya pamoja kwenye mbuyu ambapo wajerumani waliutumia kuwanyoga mababu zetu wakati wa ukoloni

Kijana michael akiwa kwenye maonesho ya nane nane, akionyesha bidhaa za kampuni yetu ya Banana Investments.